BAADA YA AKWILINA KUZIKWA, DENTI MWINGINE DAR AUAWA KINYAMA!
Shija Daudi Kasuku enzi za uahi wake.
WAKATI ripoti ya uchunguzi wa kipolisi juu ya mauaji ya aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Usafi rishaji (NIT), Akwilina Akwilini Bafta (22), ikizua gumzo kila kona kufuatia siku 14 za kuchunguza kutimia leo, tukio linguine la mauaji ya kutisha dhidi ya denti mwingine wa chuo kikuu limeshtua wengi.
Wakati Akwilina yeye aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa kwenye daladala maeneo ya Mkwajuni- Kinondoni jijini Dar, Februari 16, mwaka huu, mwanafunzi Shija Daudi Kasuku (20) wa Chuo Kikuu cha Elimu ya Biashara (CBE), Tawi la Dar, alidaiwa kuuawa kwa kusukumwa kutoka ghorofa ya tatu hadi chini.


No comments