Breaking News

REAL LOVE 💘.......SEHEMU 31


REAL LOVE 💘.......SEHEMU 31
ILIPOISHIA..........
Moyo ukaanza kunienda mbio kwani nakumbuka yule dada sikumpa namba yngu zaid ya mim kuandika namba yake bila kuisevu ,.......
ENDELEA..........
Nikaanza kuhisi jasho la hofu kwani hali haikuwa ya kawaida kwa muda ule kuwe hakuna watu, nikajikuta nakazana kuwahi nyumbani, hakika sikukawia kufika nikawa nawaza nin kinaendelea kwani leyl@th yupoje mbona simuelewi elewi,
"Sancho... "
Nilisikia nikiitwa na mama nikainuka na kuanza kuelekea chumbani kwake, nikafika nikamkuta kachoka yan akionyesha alikua amelala,
"Vip leyl@th ameondoka 😲"
"Ndiyo tena syo muda mrefu sana ,nmetoka kumsindikiza muda huu huu,
"Haya mi napumzika "
"Haya mama "
"Nikatoka nikihisi kama sijielewi elewi nikawa nahisi kizungu zungu nikaelekea kitandani nikajitupa, usingizi haukua mbali kunichokua, nilishtuka baada ya kusikia kelele za watu nje wakiitia mwizi nilipaswa kutoka kwenda kutazama mwizi gani anaiba mitaa yetu ya watu wenye roho mbaya,nilipotoka nusu nizimie kuona kundi la watu weng sana wakimkimbiza suma ambaye alionekana kuchoka sana, mapigo ya moyo yalianza kwenda mbio sana kwan nilijikuta nakimbia bila kujali ilimradi niwahi kwan alionekana kuanguka na watu walikwishaanza kumshambulia kwa mawe, mapanga, visu mwenye gongo,tofali had nilipofika mim, suma alikwishaishiwa nguvu,
"Oyaaaa Jaman huyo syo mwiz wakubwa.... 😰"niliongea kwa uchungu lakin hakuna hata aliyenitilia maanani,
Nilimshuhudia suma akikata roho kwa macho yangu huku miguu ikitapa tapa kama mtu aliyejinyonga,
"Oya kang'oka...
"Kang'oka... aaah qmmamae msala wauni... 🏃🏃"waliongea kisha wakaanza kukimbizana wakabaki watu wachache nikiwemo mim, sikuwa na jinsi zaid ya kuuchukua mwili wa rafiki yangu ambaye ni kama ndugu kwa ukaribu aliyonionyeshea, nilimpenda sana na hata yeye alinipenda sana, nikasaidiwa na baadhi ya watu wenye huruma kwan mwili wangu uliishiwa nguvu kabisa nikawa kila mara namuangusha, ilikua mida ya jioni saa 12 japo sikushangaa kutokuta hali ile niliyoiona kabla sijalala mchana, nilipofika nyumbani nilimkuta mama akiandaa chakula lkn akaacha baada ya kuona kuna msiba namletea, kwakweli alilia sana, na watu wakajaa......
********************
Ilikua jumamosi siku ya msiba wa rafiki yangu kipenz Ismail nilivalia shati jeusi alilonipatia Honestly,
Msiba uliongozwa kwa sheria zote na hatua zote za dini yetu ya kiislamu, tulipomaliza kuzika nikawa nimerudi nyumbani kwenda kukaa kupumzika kama,nilistaajabu kumuona yule dada nilikua nimepanda nae basi na alinipigia cm kwa jina alijiita Habiba, kumuona akishughulika shughulika pale nyumbani, akili ikabipa maswali msululu huku nikiwa sijui jibu hata moja........ItaEndelEaaaaa
USIKOSE REAL LOVE KUTOKA WWW.DABEST4G.BLOGSPOT.COM

No comments