Okwi, Bocco waibeba ‘Simba SC’ Taifa
Klabu ya Simba leo Jumapili Januari 28, 2018 imefanikiwa kupata ushindi
mnono wa goli 4-0 dhidi ya Majimaji FC ya Songea katika Uwanja wa Taifa
Jijini Dar es salaam.
Kutoka kulia John Bocco na Okwi wakishangilia .
Magoli ya Simba SC yamefungwa na mshambuliaji wa timu ya taifa ya
Uganda, Emmanuel Okwi goli mbili na John Bocco naye akitupia goli mbili.
Kwa matokeo hayo ya mzunguuko wa 15 wa Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara,
Simba inabaki kileleni kwa alama 35 ikifuatiwa na Azam FC yenye alama
30.

No comments